sw_tn/psa/044/018.md

1.9 KiB

Moyo wetu haujageuka ... hazijatoka kwenye njia yako

Misemo hii miwili in usambamba. Mwandishi anazungumzia uaminifu kwa Mungu kana kwamba ilikuwa kumfuata, na kutokuwa mwaminifu kana kwamba ni kumgeuka.

Moyo wetu haujageuka

Hapa neno "moyo" linamaanisha hisia, hasa za uaminifu. "Hatujaacha kuwa waaminifu kwako"

umetuvunja sana

Mwandishi anazungumzia adhabu za Mungu kana kwamba ilikuwa ni kuvunja chombo rahisi kuvunjika. "umetuadhibu vikali"

katika nafasi ya mbweha

Mwandishi anazungumzia Israeli baada ya adhabu ya Mungu kana kwamba ilikuwa sehemu ya pori, ambapo mtu hawezi kuishi. "umefanya nchi yetu kama sehemu ambayo mbweha huishi"

mbweha

aina ya mbwa pori

kutufunika na kivuli cha mauti

Mwandishi anazungumzia mauti kana kwamba ni kitu kinachotoa kivuli juu ya wale wanaotaka kufa. "umetufanya ili tuwe karibu kufa"

Kama tumesahau jina la Mungu wetu

Hapa neno "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. Kumsahau Mungu ni kuacha kumwabudu. Hili ni jambo ambalo halikutokea. "Kama tungemsahau Mungu wetu" au "Kama tungeacha kumwabudu Mungu wetu"

kusambaza mikono yetu kwa mungu mgeni

Kusambaza mikono ni ishara ambayo watu walitumia kuabudu na kuomba kwa mungu yeyote. "waliabudu mungu mgeni" au "kuomba kwa mungu mgeni"

Je, Mungu hatalichunguza hili?

Mwandishi anatumia swali hili kueleza kuwa Mungu atajua kama watamwabudu mungu mwingine. "Hakika Mungu atagundua"

anajua siri zatunauwawa siku nzima moyo

Hapa neno "moyo" unamaanisha akili na mawazo. "anajua kile ambacho mtu anawaza kwa siri"

tunauwawa siku kutwa

Msemo "siku kutwa" ni kukuza maneno kusisitiza kuwa watu wao wanauwawa mara kwa mara. "watu wanatuua kila wakati"

tumefanywa kuwa kondoo wa machinjo

"watu wanatuona kama kondoo kwa ajili ya machinjo"

kondoo wa machinjo

Mwandishi anafananisha Waisraeli na kondoo ambao watu huua na kula. Kama kondoo wasivyojiweza mbele ya wale wanaowaua, hivyo ndivyo Waisraeli wasivyojiweza mbele ya adui zao.