sw_tn/psa/042/003.md

1021 B

Machozi yangu yamekuwa chakula changu

Mwandishi anazungumzia machozi yake kana kwamba ni chakula anachokula. Hii inamaanisha kuwa ana huzuni sana hadi hawezi kula. "Machozi yangu ni kama chakula changu na sili kitu kingine"

mchana na usiku

Msemo huu unamaanisha siku nzima kwa kutaja mwanzo wake na mwisho wake. "siku nzima"

adui zangu daima wanasema kwangu

Huku ni kukuza kwa neno. Adui zake hawasemi haya muda wote; wanasema mara kwa mara.

Yuko wapi Mungu wako?

Adui wa mwandishi wanatumia swali hili kumkejeli na kuonesha kuwa hawaoni Mungu wake akimsaidia. "Mungu wako hayuko hapa kukusaidia"

itisha akilini

Hii ni lahaja inayomaanisha kuwaza au kukumbuka kitu. "kumbuka"

Ninamwaga nafsi yangu

Hapa neno "nafsi" inamaanisha hisia. Mwandishi anazungumzia nafsi yake kana kwamba ni kimiminiko anachomwaga. Msemo unamaanisha kuwa anaeleza uchungu wake wa hisia. "ninaeleza huzuni yangu"

msongamano

"kundi la watu"

furaha na sifa

Msemo huu unatumia maneno mawili tofauti kueleza wazo moja.