sw_tn/psa/039/012.md

661 B

Sikia ombi langu ... nisikilize ... sikia kilio changu

Misemo hii mitatu inamaana moja na inaonesha jinsi mwandishi anavyotaka Mungu amjibu.

Usiwe kiziwi kwangu

Mwandishi anazungumzia Yahwe kutomjibu kana kwamba ni kiziwi. "Usiache kunijali kana kwamba huwezi kunisikia"

Mimi ni kama mgeni kwako, mkimbizi

Mwandishi anazungumzia Yahwe kutomjibu kana kwamba Yahwe alikuwa akimchukulia kama mgeni kabisa kwake. "Mimi ni kama mgeni kabisa kwako"

Usinikazie macho

Hapa "kukazia macho" inawakilisha adhabu ya Yahwe. "Tafadhali acha kuniadhibu"

ili ni tabasamu tena

Hapa "kutabasamu" inahusishwa na kuwa na furaha. "ili niweze kuwa na furaha tena"