sw_tn/psa/037/031.md

788 B

Sheria ya Mungu wake moyoni mwake

Hapa "moyo" unamaanisha hali yake ya ndani zaidi. "Anathamini amri za Mungu wake ndani mwake"

miguu yake haitateleza

Kushindwa kwake kumtii Yahwe kunazungumziwa kama kuteleza kwenye njia salama au kuanguka. "atatembea salama katika njia ambayo Mungu anataka atembee" au "atafanya kwa usalama vitu ambavyo Mungu anataka afanye"

Mtu mwovu ... mtu mwenye haki ... mtu mwovu

Hawa sio watu bayana. Inamaanisha aina hii ya watu kwa ujumla.

humtazama mtu mwenye haki

Hapa kutazama inaashiria kuwaangalia wenye haki ili kuwadhuru. "husibiri ili kumvamia mtu mwenye haki"

mkono wa mtu mwovu

Hapa "mkono" unawakilisha uwezo au nguvu. "uwezo wa mtu mwovu"

anapohukumiwa

Hii inamaanisha Yahwe kumhukumu mtu mwenye haki. "Yahwe atakapomhukumu"