sw_tn/psa/034/012.md

852 B

Kuna mtu gani anayetamani maisha na kupenda siku nyingi, ili aone mema?

Jibu linalodokezwa la swali hili ni "kila mtu." Swali hili balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kila mtu anatamani maisha na anatamani kuishi siku nyingi na kuwa na maisha mazuri"

weka ulimi wako mbali na uovu ... weka midomo yako mbali na kuongea uongo

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasemwa katika njia tofauti ili kusisitiza umuhimu wake.

Basi weka ulimi wako mbali na uovu

Hapa "ulimi" inamaanisha mtu mzima. "Basi, usizungumze uongo"

weka midomo yako mbali na kuongea uongo

Hapa "midomo" inamaanisha mtu anayezungumza. "usizungumze uongo"

Ugeuke uovu

Hapa "ugeuke" ni sitiari ya kuepuka na uovu. "Kataa kufanya uovu"

Tafuta amani

Hapa "kutafuta" inamaanisha kujihusisha na amani. "Jaribu kwa bidii kuishi kwa amani na watu wengine"