sw_tn/psa/033/004.md

789 B

Taarifa ya Jumla:

Kila mstari una mistari miwili yenye maana za kufanana.

Neno la Yahwe ni imara

Hapa "imara" ni sitiari kwa jambo lililo la kweli. "Yahwe daima hufanya anachosema atafanya"

Anapenda haki na hukumu

Nomino hizi dhahania zinaweza kuelezwa kama vitendo. "Anapenda kufanya kilicho cha haki na sawa" au "Anawapenda wale wanaofanya kilicho cha haki na sawa"

Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe

Hapa "Dunia imejaa" ni lahaja inayomaanisha kwamba uaminifu wa agano unaweza kuonekana duniani kote. "Uaminifu wa agano la Yahwe unaweza kupitia duniani kote"

Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa kutumia neno lake, Yahwe aliziumba mbingu"

kwa pumzi ya mdomo wake

Hii inamaanisha neno la Yahwe. "kwa neno lake"