sw_tn/psa/028/001.md

1.0 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

ninalia

"ninaita kwa sauti"

mwamba wangu

Hii ni sitiari ya nguvu. "nguvu yangu"

usiache kunijali

"usiwe kimya kwangu" au "usiniache mwenyewe"

Nitaungana na wale wanaoenda chini kaburini

Watu wanaokufa wanazungumziwa kana kwamba wanaenda kaburini. "Nitakufa kama wale waliomo kaburini"

Sikia sauti ya dua yangu

Hapa "sauti" inamaanisha maneno ya ombilake. "Sikia ombi langu kuu"

Napainulia mikono yangu mahali pako patakatifu

Kuinua mikono ni ishara ya kuabudu. Mwandishi haabudu mahali patakatifu, bali Yahwe anayeishi katika sehemu hiyo takatifu.

mahali pako patakatifu

Maana zinazowezekana ni 1) kama Daudi aliandika hii, basi hii inamaanisha hema ambalo Mungu aliwaambia watu wake kuandaa ili wamwabudu humo, au 2) kama ni mtu aliandika baada ya wakati wa Daudi, basi mwandishi anamaanisha hekalu lililoko Yerusalemu.