forked from WA-Catalog/sw_tn
888 B
888 B
Nani ataupanda mlima ... katika sehemu yake takatifu?
Maswali yote haya mawili ya maana moja. Mwandishi anauliza kuhusu nani anayefaa kwenda kumwabudu Yahwe.
kupanda
"kwenda juu"
mlima wa Yahwe
Hii inamaanisha mlima Sayuni ndani ya Yerusalemu
sehemu yake takatifu
Hii inamaanisha hekalu la Yahwe. Hekalu lake liko katika mlima Sayuni ulioko Yerusalemu.
Yeye aliye ...aliye ... na haja...
Hapa haimzungumzii mtu bayana. "Wale ambao ...walio ... na hawaja..."
aliye na mikono safi
Neno "mikono" inawakilisha kile ambacho mtu anafanya. Kwa "mikono" kuwa safi inamaanisha anafanya kilicho sawa. "anafanya kilicho sawa"
moyo safi
Hapa "moyo" inamaanisha mawazo au nia ya mtu. "anawaza mawazo mazuri" au "hawazi kuhusu yaliyo mabaya"
ambaye hajainua juu uongo
Hapa "uongo" inawakilisha sanamu ya uongo. "Kuinua juu" inamaanisha kuabudu. "ambaye hajaabudu sanamu"