sw_tn/psa/023/004.md

800 B

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii inaendelea kueleza jinsi Mungu anavyotujali kama mchungaji anavyojali kondoo wake.

Ingawa ninatembea katika bonde la kivuli cha giza zaidi

Mwandishi anamwelezea mtu anayepitia matatizo makubwa kana kwamba ni kondoo anayetembea kwenye bonde hatari la giza. Huko kondoo anaweza kupotea au kuvamiwa na mnyama pori. "Ingawa maisha yangu ni kama kutembea katika bonde hatari la giza"

sitaogopa madhara

Nomino dhahania ya "madhara" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Sitaogopa kitu kunidhuru"

uko nami

Aliye pamoja naye ni Yahwe.

gongo lako na fimbo yako hunifariji

Gongo na fimbo inaashiria ulinzi kwa sababu wachungaji walizitumia kuwalinda kondoo wao kutoka hatarini. "Siogopi kwa sababu unanilinda kama mchungaji anavyolinda kondoo wake kwa gongo na fimbo"