sw_tn/psa/022/028.md

839 B

Kwa kuwa ufalme ni wa Yahwe

Hapa "ufalme" unaashiria utawala wa Mungu kama mfalme. "Kwa kuwa Yahwe ni mfalme"

yeye ni mtawala juu ya mataifa

Hapa "mataifa" yanaashiria watu wa mataifa. "anawatawala watu wa mataifa"

wata kuwa na karamu

Watu watakula pamoja kwenye karamu. "watakula pamoja" au "watakula chakula cha sherehe pamoja"

wale wote wanaoenda chini kwenye vumbi ... wale ambao hawawezi kuhifadhi maisha yao wenyewe

Misemo hii miwili inaashiria kundi moja. Zote zinamaanisha watu wote kwa kuwa watu wote watakufa.

wale wote wanaoshuka kwenye vumbi

Hapa "vumbi" linamaanisha kaburi. Msemo "wanaoshuka kwenye vumbi" ni njia ya kusema mtu anakufa. "wale wanaokufa" au "wale waliokufa"

wale ambao hawawezi kuhifadhi maisha yao wenyewe

"wale ambao hawawezi kuokoa maisha yao" au "wale ambao hawawezi kujizuia kufa"