sw_tn/psa/009/007.md

626 B

Yahwe anabaki milele

"Kubaki" inaweza kuashiria kuketi kwenye kiti cha enzi kama mfalme. "Yahwe anaketi kwenye kiti chake cha enzi milele" au "Yahwe anatawala milele"

ameweka kiti chake cha enzi kwa jili ya haki

Msemo "kiti chake cha enzi" unaashiria utawala wa Mungu. Maana zinazowezekana ni 1) "Anatawala ili ahukumu watu" au "Anatawala juu ya watu kwa haki"

Atahukumu ulimwengu kwa haki ... atatekeleza hukumu kwa ajili ya mataifa kwa kutopendelea.

Vishazi hivi viwili vinaeleza kitu kimoja.

Atahukumu ulimwengu kwa haki

Hapa "ulimwengu" unamaanisha watu wote duniani. "Atahukumu watu wote duniani kwa haki"