sw_tn/psa/003/007.md

878 B

Inuka

Daudi anazungumzia kuanza kufanya kitu kama kuinuka. "Chukua hatua" au "Fanya kitu"

utawapiga maadui wangu wote ... utavunja meno ya waovu

Vifungu hivi vinasema vitu vya kufanana sana. Misemo "maadui wangu" na "waovu" inamaanisha kundi moja la watu.

Kwa kuwa utawapiga maadui wangu kwenye taya

Hii ilikuwa ni njia ya kuwatukana watu. Daudi anazungumza kana kwamba Yahwe atakuja na kuwapiga kimwili adui zake. "Kwa kuwa utawafedhehesha adui zangu wote kama mtu anawapiga kwenye taya.

utavunja meno ya waovu

Wanyama huvamia kwa meno yao. Kuvunja meno yao inawaondolea nguvu ya kuvamia. Daudi anazungumza kana kwamba Yahwe atakuja na kupambana kimwili na waovu. "utawafanya waovu washindwe kunidhuru kama mtu kuvunja meno ya mnyama mkali"

Wokovu unatoka kwa Yahwe

Nomino dhahania ya "Wokovu" inaweza kuelezwa na kitenzi "okoa." "Yahwe anawaokoa watu wake"