sw_tn/psa/003/003.md

920 B

wewe, Yahwe, ni ngao yangu

Ngao humlinda askari. Daudi anazungumza kana kwamba Mungu ni ngao inayomlinda. "wewe, Yahwe, unanilinda kama ngao"

utukufu wangu

"wewe ni utukufu wangu." Kwa kumuita Mungu utukufu wake, Daudi anasema kuwa Mungu ndiye anayempa utukufu. Kwa kuwa Daudi amemaliza tu kuwazungumzia maadui zake na Mungu kuwa mlinzi wake, inawezekana alimaanisha kuwa Mungu anampa utukufu kwa kumpa ushindi juu ya maadui wake. "wewe ndiye unipaye utukufu" au "wewe ndiye unipaye ushindi"

unayenyanyua kichwa changu

"wewe ndiye unayenyanyua kichwa changu." Kumpa mtu ujasiri inazungumziwa kama kumnyanyua kichwa chake. "unayenitia moyo"

Nainua sauti yangu

Mtu kutumia sauti yake kulia inazungumziwa kama kuinua sauti yake.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.