sw_tn/psa/002/001.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa nini mataifa yako katika ghasia ... kwa nini watu wanafanya mipango itakayoshindwa?

Vishazi hivi viwili vina maana zakufanana, na "mataifa" na "watu" linamaanisha kundi hilo hilo la watu. Maneno "mataifa" na "watu" yanaweza kumaanisha viongozi wao. "Kwa nini viongozi wa mataifa wako katika ghasia na kufanya mipango itakayoshindwa?"

Kwa nini mataifa yako katika ghasia, na kwa nini watu wanafanya mipango itakayoshindwa?

Maswali haya yanatumika kuonesha mshangao kwamba watu wanafanya jambo baya sana na laki pumbavu. "Mataifa yako katika ghasia na watu wanafanya mipango itakayoshindwa."

mataifa yako katika ghasia

Hii inaweza kumaanisha kuwa mataifa yalikuwa yakifanya vurugu ya kelele na hasira.

mipango itakayoshindwa

Hii inawezekana kuwa mipango dhidi ya Mungu na watu wake.

Wafalme wa nchi wafanya msimamo wa pamoja ... viongozi wao wanafanya njama pamoja.

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana.

wafanya msimamo wa pamoja

"kukusanyika kupambana" au "kuungana na kujiaanda kupinga"

Tupasue pingu ... tutupe minyororo yao

Watu wa mataifa mengine wanamzungumzia utawala wa Yahwe na Masihi juu yao kama pingu na minyororo. "Tujiweke huru kutoka kwenye utawala wao; tusiwaruhusu watutawale tena!"