sw_tn/psa/001/001.md

725 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

ambaye hatembei katika ushauri wa waovu

"Ushauri wa waovu" unazungumziwa kana kwamba ni njia ya kufuata. "ambaye hafuati ushauri wa waovu"

kusimama katika njia ya watenda dhambi

Hapa neno "njia" inaonesha namna watu wanavyoishi. Neno "simama" liko sambamba na "tembea." "kuiga tabia za watu watenda dhambi"

au kuketi katika kusanyiko la wenye dhihaka

Kuketi na watu wanao mdhihaki Mungu inaonesha kuwaunga watu wanao mdhihaki Mungu. "au kuwaunga wale wanao mdhihaki Mungu" au "au kumdhihaki Mungu na wale wanaomdhihaki"

furahi

"kuridhika" au "furaha"

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la kale.