sw_tn/mrk/14/22.md

952 B

mkate

Huu ulikuwa ni mkate ulio bapa ambao haujatiwa chachu, ambao uliliwa kama sehemu ya chakula cha pasaka

kuumega

Hii inamaanisha kwamba aliumega katika vipande ili kwamba watu wale.

Alichukua kikombe

Hapa "kikombe" ni kirai cha mvinyo. "Alichukua kikombe cha mvinyo"

Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi

Agano ni kwa ajili ya msamaha wa dhambi. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Hii ni damu yangu ambayo inathibitisha agano, damu imwagikayo ili kwamba wengi wapokee msamaha wa dhambi"

Hii ni damu yangu

"Mvinyo huu ni damu yangu. Ni vizuri kutofasiri kihalisia, ijapokuwa wengi huelewa hii kumaanisha kwamba mvinyo unawakilisha damu ya Yesu na huo mvinyo si damu halisi.

Kweli nawaambia

Hii inaonyesha kuwa sentensi inayofuata hasa ni kweli na muhimu.

zao hili la mzabibu

"mvinyo" Hii ni njia ya maelezo inayorejea kwa mvinyo.

mpya

Maana zinazowekana ni 1) "tena" au 2)"kwa njia mpya"