sw_tn/mrk/02/22.md

1008 B

Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu

Yesu analinganisha mafundisho yake na wanafunzi wake na divai mpya na viriba vipya. Mfano huu hujibu swali "Kwa nini wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi? Hapa "Hakuna mtu akabidhiye mafundisho mapya kwa wale waliozoea mafundisho ya zamani."

Divai mpya

"juice ya zabibu." Hii ina maana ya mvinyo ambayo haijaumuka bado. Kama zabibu hazijulikani katika eneo lako, tumia neno la jumla kwa matunda.

virriba vikuukuu

Hii inamaanisha viriba ambavyo vimetumika mara nyingi

viriba

Hii ilikuwa mifuko iliyotengenezwa kwa kutumia ngozi za wanyama. Pia inaweza kuitwa "mifuko ya divai" au "mifuko ya ngozi" (UDB)

divai itaweza kuvipasua viriba

Wakati divai mpya inapoumuka na kupanuka, inaweza kupasua na kutoka nje kwa sababu havitaweza tena kunyooka kwa nje.

kupotea

kuharibika

viriba vipya

"viriba vipya" au "mifuko mipya ya divai." Hii inarejea kwa viriba vipya ambavyo havijawahi kutumika.