sw_tn/mrk/02/17.md

935 B

Sentensi unganishi

Yesu aliitikia kwa kile walichokuwa wamesema waandishi kwa wanafunzi wake kuhusu kula na watoza kodi na watu wenye dhambi.

aliwaambia

aliwaambia waandishi

Watu walio na nguvu katika mwili hawamhitaji tabibu; ni wagonjwa pekee ndio wanamhitaji

Yesu aliwalinganisha wale wanajijua kuwa ni wenye dhambi na wale wale wanaojijua kuwa ni wagonjwa. "Watu wanaofikiri kuwa wao ni wenye haki hawahitaji msaada; ni wale tu wanaojijua kuwa ni wagonjwa ndio wanaohitaji msaada!

nguvu katika mwili

"afya"

Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi

Yesu alitegemea kuwa wasikilizaji wake wangeelewa kwamba alikuja kwa wale wanaohitaji msaada. "Nilikuja kwa watu wanaojielewa kuwa ni wenye dhambi, siyo kwa watu wanaoamini kuwa wao ni wenye haki."

lakini watu wenye dhambi

Inaweza kuwa msaada kutaja kwamba hii inarejea kwa watu ambao Yesu aliwaita. "lakini nilikuja kuwaita watu wenye dhambi"