sw_tn/mrk/02/08.md

985 B

katika roho yake

"ndani ya utu wa ndani" au"ndani yake"

walikuwa wakifiri miongoni mwao wenyewe

Waandishi walikuwa wakifiri kila mmoja nafsini mwake; walikuwa hawaongeleshani kila mmoja na mwenzake.

Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

Yesu aliuliza swali hili kuwakemea waandishi kwa kutilia mashaka mamlaka yake. NI kama alitaka kusema kuwa, "Hampaswi kuonea shaka mamlaka yangu!"

hii iko ndani ya mioyo yenu

Neno "mioyo" linatumika mara kwa mara kurejea kwenye mawazo, hisia, matamanio, au mapenzi ya mtu

Lipi ni jepesi kusema kwa mtu aliyepooza... chukua kitanda, na utembee?

Yesu aliuliza swali hili kwa sababu waandishi waliamini kwamba mtu huo alikuwa amepooza kwa sababu ya dhambi zake na ikiwa dhambi za mtu huyo zingesahewa, angeweza kutembea. Kama Yesu alimponya mtu aliyepooza, waandishi walipaswa kukiri kwamba Yesu anaweza kusamehe dhambi. Sawa na kusema "Ni rahisi kumwambia mtu aliyepooza dhambi zako zimesamehewa!" [Hili ni swali lisihitaji jibu]