sw_tn/mat/22/15.md

1009 B

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya viongozi wa dini wakipanga jinsi ya kumkamata Yesu kwa kutumia maswali mengi magumu. Hapa Mafarisayo wanamuuliza Yesu juu ya kulipa kodi kwa Kaisari.

Jinsi ya kumkamta Yesu katika maneno yake mwenyewe.

"Jinsi ambavyo wangeweza kumsababisha Yesu kukosea katika kauli ili wamkamate"

wanafaunzi wao ... Maherode

Wanafunzi wa Mafarisayo walikubaliana na swala kulipa kodi kwa mamlaka za Kiyahudi. Maherode walikubaliana na swala la kulipa kodi kwa mamlaka za Kirumi. kwa maana hiyo, Mafarisayo waliamini kuwa kwa vyote ambavyo Yesu angejibu; angelikosea moja ya makundi hayo.

Maherode

Hawa walikuwa wafuasi na maofisa wa Herode mfalme wa Wayahudi. Alikuwa rafiki wa mamlaka za Kirumi.

Hauoneshi upendeleo kwa watu.

"Huoneshi heshima ya kipekee kwa baadhi ya watu" au " haujali tu watu maarufu zaidi."

Kulipa kodi kwa kaisari

Watu hawakulipa kodi moja kwa moja kwa Kaisari lakini kwa mmoja wa maofisa wake. "Kulipa kodi ambayo Kaisari alilitaka"