sw_tn/mat/11/18.md

2.0 KiB

Sentensi unganishi:

Yesu anahitimisha kuongea na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji.

bila kula mkate au kunywa mvinyo

Hapa "mkate" unamaanisha chakula. Haimanishi kuwa Yohana alikuwa hali chakula. Inamaanisha kuwa alikuwa anafunga mara kwa mara na alipofungua hakula vizuri, chakula cha gharama. "Mfungo endelevu na kutokunywa pombe" au "kutokula chakula kizuri na kutokunywa divai"

walisema, 'ana pepo.'

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya mojakwa moja. ''wanasema kwamba ana pepo'' au ''walimtuhumu kuwa na pepo.''

wanasema

Matukio yote ya "wali" yanamaanisha watu wa kizazi kile, na zaidi sana mafarisayo na viongozi wa dini.

Mwana wa Adamu

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe. " Mimi mwana wa Adamu"

alikuja akila nakunywa

Hiki ni kinyume cha tabia ya Yohana. Hii ni zaidi ya kula kiasi cha kawaida cha chakula na kinywaji. Inamaanisha Yesu alisherehekea na kufurahia chakula na kinywaji kizuri kama vile watu wengine walivyofanya.

wakasema, anagalia, ni mtu mlaji

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "wanasema kuwa ni mlaji" "wanamtuhumu kuwa anakula sana" Kama ulitafasiri "Mwana wa mtu" kama "Mimi, Mwana wa mtu," Ile nukuu ya moja kwa moja inaweza kutafsiriwa kama "wanasema kwamba mimi ni mlaji"

mlevi

"mlevi" au "hunywa pombe nyingi daima."

Lakini hekima huthibitishwa kwa mataendo yake

Hii ni mithali ambayo Yesu anaitumia katika mazingira haya, kwa sababu watu waliomkataa yeye na Yohana walikuwa hawapati hekima. Yesu na Yohana mbatizaji ni watu wa hekima, na ,matokeo ya matendo yao yanathibitisha.

Hekima huthibitiswa kwa matendo yake

Hapa "hekima" imefafanuliwa kama mwanamke aliyethibitishwa kuwa ni mwema kwa matendo yake. Yesu anamaanisha kuwa matokeo ya matendo ya mtu huthibitisha kuwa ni mwenye hekima. "Hii inawza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Matokeo ya matendo ya mtu humthibitisha kuwa ni mwenye hekima"

hekima inaonekana

Haya maelezo, Yesu anafafanua hekima kama vile ilikuwa ni mwanamke, haitumiki hapa kwa namna kwamba hekima inatoa haki mbele ya Mungu ila kwamba hekima inaonekana haki.