sw_tn/mat/11/16.md

1.4 KiB

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuongea na makutano juu ya Yohana Mbatizaji.

Nikilinganishe na nini

Yesu anaitumia swali kutoa mlinganisho kati ya watu wa nyakati zile na kile amabacho watoto wanaweza kusema katika eneo la soko. "Hivi ndivyo kizazi hiki kilivyo"

kizazi hiki

''watu wanaoishi sasa'' au ''watu hawa'' au ''ninyi watu wa kizazi hiki''

Ni mfano wa watoto wanaocheza maeneo ya sokoni ... na hamkulia

Yesu anatumia mfano kuwaelezea watu waliokuwa hai kipindi hicho. Anawalinganisha na kikundi cha watoto wanaojaribu kuwavuta watoto wengine ili wacheze nao. Lakini haijarishi aina ya mbinu yeyote wanayotumia, wale watoto wengine hawataungana nao. Yesu anamaanisha kuwa haijalishi kama Mungu alimtuma mtu kama Yohana mbatizaji, anaishi nyikani na kufunga, au mtu kama Yesu, ambaye anasherehekea na wenye dhambi bila kufunga. Watu, hususani Mafarisayo na viongozi wa dini, bado wanabaki wasumbufu na wanakataa kuupokea ukweli wa Mungu

maeneo ya soko

eneo kubwa, la wazi ambapo watu walikuja kuuza na kununu bidhaa zao.

tuliwapigia zomari

''tu'' inarejelea watoto waliokuwa wamekaa katika maeneo ya soko. ''wa'' ni wingi na inarejelea lile kundi lingine la watoto

na hamukucheza

''lakini hamukucheza ule muziki mzuri''

tuliomboleza

Hii inamaanisha waliimba nyimbo za huzuni kama vile wanawake wafanyavyo kwenye mazishi.

na hamukulia

''lakini hamukulia pamoja nasi''