sw_tn/mat/10/11.md

2.0 KiB

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu nini wanachopaswa kufanya watakapoenda kuhubiri.

mta...yenu

Hivi viwakilishi vinaonyesha mitume kumi na wawili

Kwa kila mji au kijiji mtakachoingia

"Kwa "Kila mji au kijiji" mtakachokwenda" au

Mji..kijiji

"kijiji kikubwa...kijiji kidogo" au "mji mkubwa...mji mdogo." Tazama ilivyotafsriwa katika 9:35.

anayestahili ... asiyestahili

Katika 10:11-13 "anayestahili" inamaanisha mtu aliyetayari kuwakaribisha wanafunzi wa Yesu. Yesu anamlinganisha mtu asiyekuwa tayari kuwakaribisha wanafunzi wake saw namtu asiyestahili

mkae pale mpaka mtakapoondoka

Maana halisi ya sentensi hii inaweza kuwa sahihi kama itasemwa "mkae katika nyumba ya huyo mtu mpaka mtakapoondoka kwenye huo mji au kijiji"

Mtakapoingia katika nyumba,salimuni

Kirai cha "salimieni" inamaanisha isalimuni hiyo nyumba. Salamu ya kawaida kwa nyakati zile ilikuwa "amani iwe katika nyumba hii. "Kaya" inamaanisha watu wanao ishi kwenye hiyo nyumba. mkiwa mnaingia kwenye nyumba, muwasalimu watu wanaoishi ndani yake.

nyumba inastahili

"Nyumba" inamaanisha wale wanaoishi kwenye hiyo nyumba. "watu wanaoishi kwenye nyumba hiyo wakiwakaribisha vizuri" au kaya ile iwakiwakarimu vizuri"

amani yenu ibaki pale

Neno "pale" linamaanisha kaya. Nyumba hapa inamaanisha watu wanaoishi kwenye hiyo nyunba. Amani yenu ibaki pale" au "watu wanaoishi katika nyumba ile wataishi katika amani"

amani yenu

Hii ni amani ambayo mitume wanapaswa kumwomba Mungu awape wanaoishi katika nyumba.

Kama haistahili

Neno "pale" linamaanisha nyumba . "Nyumba" inamaanisha kaya. "ikiwa hawatawakaribisha vizuri" au ikiwa hawatawakarimu"

amani yenu iondoke pamoja nanyi

Yamkini ina maana zifuatazo: 1) Ikiwa nyumba haistahili, ndipo Mungu atazuia amani au baraka katika nyumba hiyo au 2) Ikiwa kaya haistahili, ndipo mitume walipaswa kufanya kitu, kama vile kumwomba Mungu asikubali heshima ya salaam za amani. Ikiwa lugha yako ina maana kama hii ya kurudisha salaam au matokeo, hivyo itumike hapa.