sw_tn/mat/10/05.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Hapa Yesu anaanza kutoa maelekezo kwa wanafunzi wake juu ya jinsi wanavyopaswa kufanya na wategemee nini wakienda kuhubiri.

Maelezo kwa ujumla

Ijapokuwa mstari wa tano unaanza kwa kusema kuwa alaiwatuma thenashara, Yesualiwapa maelekezo haya kabla ya kuwatuma.

Hawa kumi na wawili Yesu aliwatuma

"Yesu aliwatuma hawa wanaume kumi na wawili" au "Walikuwa ni hawa wanaume kumi na wawili ambao Yesu aliwatuma"

aliwatuma

Yesu aliwatuma kwa kusudi maalumu.

Naye akawaelekeza wao

"Naye aliwaambia kitu gani walipaswa kutenda" au "aliwaamuru wao"

Kondoo aliyepotea wa nyumba ya Israel

Hiki ni kirai kinacholinganisha taifa zima la israel na kondoo ambao wamejitenga kutoka kwa mchungaji

nyumba ya Israel

Haya maelezo yana maanisha taifa la Israel. "watu wa Israel" au "kizazi cha Israel"

Mnapokwenda

Kiwakilishi "mna" ni cha wingi na kinamaanisha mitume kumi na wawili.

Ufalme wa mbinguni umekaribia

Hiki kirai cha "ufalme wa mbinguni", kinapatikana katika injili ya Mathayo tu. Kinamaanisha Mungu ni mfalalme. kama inawezekana tumia neno "mbinguni" katikatafsiri zako. "Mungu wetu wa mbinguni atajidhihirisha mapema kuw a yeyeni mfalme. Tazama ilivyotafsiriwa katika 3:1