sw_tn/mat/09/35.md

1.0 KiB

Sentensi unganishi

Mstariwa 35 ni mwisho wa sehemu ya simulizi ambayo imeamnzia katika 8:1 kuhusu huduma ya Yesu ya uponyaji kule Galilaya.

Maelezo kwa ujumla

Mstari wa3 6 unaanzisha sehemu nyingine ya simulizi ambapo Yesu anawafundisha wanafunzi wake na kuwatuma kwenda kuhubiri na kuponya kama alivyokuwa akifanya.

miji yote

Yesu alienda kwa wengi au kwa miji mingi lakini si kwa kila mji. "Katika miji mingi"

miji....vijiji

"vijiji vikubwa...vijiji vidogo" au "miji mikubwa...miji midogo"

injili ya ufalme

Hapa neno "Ufalme" linamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. tazama ilivyotafsiriwa karika 4:23

magonjwa ya kila aina na udhaifu wa aina zote

"kila magonjwa na kila udhaifu" Neno "magonjwa" na "udhaifu" yanakaribiana kufanana lakini yanapaswa kutafsiliwa tofauti kama inawezekana. "Ugonjwa" unamfanya mtu kuwa dhaifu. "Udhaifu" kukosa nguvu mwili au tokeo linalosababishwa na kuwa na ugonjwa.

Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji

Mfanano huu unamaanisha kuwa hawakuwa na kiongozi wa kuwaangalia. "Watu hawakuwa na kiongozi"