sw_tn/mat/06/22.md

1.1 KiB

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafasi. viwakilishi vya "yako" vimo katika umoja lakini waweza kuvitafsiri katika wingi.

Jicho ni taa ya mwili... hilo giza ni kubwa kiasi gani

Hii inalinganisha macho mazima ambayo yanamwezesha mtu kuona macho mabovu ambayo yanasababisha mtu kuwa kipofu. Huu ni msemo unaomaanisha uzima wa kiroho. Mara nyingi, wayahudi walitumia msemo "macho mabaya" wakimaanisha uovu. Maana yake ni hii ikiwa mtu amejitoa kwa Mungu na kuona vitu vinafanyika kwa njia hiyo wanafanya vizuri. Endapo mtu ana tamaa ya utajiri wa vitu vingine hivyo anafanya uovu.

jicho

Unaweza kutafsiri kwa wingi, "macho"

ikiwa jicho lako ni baya

Hii aimanishi maajabu. Wayahudi mara zote walitumia msemo huu kwa mtu ambaye ni mwovu.

kwa kuwa atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au la sivyo atajitoa kwa mmoja na kumwachaniza mwingine

Yote kwa pamoja kimsingi yana maana moja. Yanasisitiza kwamba mtu hawezi kupenda na kujitoa kwa Mungu na fedha kwa wakati mmoja.

Huwezi kumtumikia Mungu na mali

"Huwezi kumpenda Mungu na fedha kwa wakati mmoja"