sw_tn/mat/06/16.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya kufunga

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika maisha yao binafsi. Viwakilishi vyote vya "una" na "zao" katika mstari wa 17 na 18 viko katika umoja, lakini vinaweza kutafsiriwa katika wingi ili vioane na kile cha "wa" katika mstari wa 16.

Aidha

"Zaidi ya"

wanakunja sura zao

Wanafiki hawakuosha nyuso zao au kuchana nywele zao. Walifanya hivyo makusudi kuvuta hisia zao ili kwamba watu wawatazame wao na kuwapa heshima kwa sababu ya kufunga.

kweli ninakuambia

"Ukweli ninakuambia." Huu msemo unaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakiongea baadaye.

tengeneza kichwa chako

"paka mafuta kwenye nywele zako" au "tengeneza nywele zako" Kutunza kichwa hapa ni hali ya kawaida ya kutunza nywele. Halina uhusiano na "Kristo" ikimaanisha "mpakwa mafuta" Yesu alikuwa anamaanisha kwamba watu wanapaswa kuonekana kawaida haijalishi wamefunga au hawakufunga.

Baba aliye sirini ... yeye anayeona sirini

Tazama unavyotafsiri hii kwenye 6:5

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

aonaye sirini

"Aonaye kile unachokifanya unapokuwa pekee yako" Tazama ilivyotafsriwa katka 6:5