sw_tn/mat/05/38.md

1.5 KiB

sentnsi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Anaanza kwa kuongelea juu ya kisasi kwa maadui

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya mtu kibinafsi. Kiwakilishi cha "mme" katika "mmesikia" na "mimi nawaambia" viko katika wingi. Kirai hiki "mtu akikupiga" kimesemwa katika umoja "akiku...," lakini unaweza kukitafsiri katika wingi "akiwa..."

mmesikia imenenwa kuwa

Yesu anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini hakubaliani na jinsi viongozi wa dini walivyolitumia neno la Mungu. "Viongozi wenu wa dini wamewambieni kuwa Mungu alisema." Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:33

jicho kwa jicho na jino kwa jino

Sheria ya Musa ilimruhusu mtu kumwumiza kwa njia ileile kama alivyomwumiza, lakini hakumwumiza zaidiya kiasi kile

Lakini mimi nawaambia

Kiwakilishi cha "mimi" kinaongeza msisitizo. Hii inamaanisha kuwa alichosema Yesu kina umuhimu sawa na ule ulio kwenye amri kuu kuto kwa Mungu. Jaribu kutafsiri kirai hiki katika namna ambayo italeta msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa 5:21.

mtu mwovu

"ni mtu mwovu" au "mtu yeyote aliyewahi kukuumiza"

akikupiga shavu la kulia

Kumpiga mtu upande mmoja wa uso kilikuwa kitendo cha fedheha katika utamaduni wa Yesu. Kama ilivyo katika jicho na mkono, shavu la kulia ni la muhimu, kwa hiyo kukupiga shavu la kulia ilikuwa fedhaha kubwa mno.

akikupiga

"kuzabua," hii inammanisha kupiga kumpiga mtu kofi kwa ubapa wa mkono,

mgeuzie na jingine tena

"mwache akupige na shavu jingine pia"