sw_tn/mat/05/19.md

990 B

yeyote avunjaye

"yeyote asiyetii" au "yeyote apuuziaye"

amri ndogo mojawapo ya amri hizi

"yeyote kati ya amri hizi, hata zile ndogo kabisa"

ataitwa

Hii inaweza kuelezeka kwa muunda tendaji. "Mungu atamwita mtu huyo" au "Mungu atawaita watu hao".

mdogo katika ufalme wa mbinguni

Kirai hiki kimetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana tumia "mbingu" katika tafsiri yako. "asiye na umuhimu kabisa kwenye ufalme wa Mungu" au "asiye na umuhimu katika utawala wa Mungu wetu wa mbingunij".

azishikaye na kuzifundisha

"anayetii amri zote hizi na kuwafundisha wengine kufanya hivyo hivyo"

mkubwa

"wa muhimu zaidi"

Kwa maana nawaambia

Hiki kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu atasema baadaye.

nawa ... yenu ... hamta..

hivi ni viwakilishi vya wingi

haki yenu isipozidi haki ya waandishi n a mafarisayo, kwa vyovyote vile hamtaingia kataika ufalme wa mbinguni

Hii inaweza kuelezeka kwa muundo hai. "kwamba haki yenu lazima izidi... ili kuingia"