sw_tn/mat/04/23.md

1.1 KiB

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu mwanzo wa huduma ya Yesu Galilaya. Mistari hii ni muhtasari wa kile alichofanya na jinsi watu walivyoitikia.

kufundisha katika masinagogi yao

"kufundisha katika masinagogi ya Wagalilaya" au kufundisha katika masinagogi ya watu wale"

kuhubiri injili ya ufalme

Hapa "ufalme" humaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "kuhubiri habari njema kuhusu jinsi Mungu atakavyojifunua mwenyewe kama mfalme."

"aina zote za maradhi na aina zote za magonjwa"

"kila maradhi na kila ugonjwa." Maneno "maradhi" na :magonjwa" yanakaribia sana lakini yanapaswa kutafsiriwa kama maneno mawili tofauti kama inawezekana. "Maradhi ni kile kinacho sababisha mtu kuwa mgonjwa. "Ugonjwa ni udhifu wa mwili au maumivu ambayo ni matokeo ya kuwa na maradhi.

wale waliopagawa na pepo

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "walio na pepo" au "wale ambao wanatawaliwa na pepo."

wenye kifafa

"wale waliokuwa na kifafa" au wale walio na maradhi ambayo yalisababisha kuzirai."

waliopooza

"wale ambao hawakuweza kutembea"

Dekapoli

Jina hili humaanisha "Miji Kumi."