sw_tn/mat/04/14.md

1.1 KiB

Taarifa kwa ujumla:

Katika mstari wa 15 na 16, mwandishi anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba huduma ya Yesu Galilaya ilikuwa ni kutimizwa kwa unabii.

Hii ilitokea

Hii inamaanisha Yesu kwenda kuishi Kaperenaumu.

kilichonenwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "kile Mungu alichonena"

Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali...Galilaya ya Wamataifa.

Majimbo haya yote yanaeleza eneo lilelile. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi timilifu. "Katika jimbo la Zabuloni na Naftali...katika jimbo hilo huishi Wamataifa wengi."

kuelekea bahari

Hii ni bahari ya Galilaya.

Watu waliokaa katika giza wameona mwanga mkuu

Hapa "giza" humaanisha maisha ya gizani au dhambi ambayo huwatenga watu na Mungu. Na "mwanga" humaanisha ujumbe wa kweli wa Mungu ambao huwaokoa watu kutoka katika dhambi yao. Hii ni taswira ya watu ambao hawa kuwa na tumaini sasa wana tumaini kutoka kwa Mungu.

kwa hao ambao walikaa katika eneo na kivuli cha kifo, juu yao mwanga umewazukia

Kimsingi hii ina maana ileile kama sehemu ya kwanza ya sentensi. Hapa "eneo" na kivuli cha kifo" humaanisha kifo cha kiroho au kutengana na Mungu.