sw_tn/mat/03/10.md

2.3 KiB

Maelezo yanyounganisha

Yohana Mbatizaji anaendelea kuwakemea Mafarisyo na Masadukayo.

Tayari shoka limekwisha wekwa kwenye shina la miti. Hivyo kila mti usioweza kuzaa matunda mazuri unakatwa na kutupiwa motoni.

Sitiari hii inamaanisha Mungu yuko tayari kuawaadhibu wenye dhambi. Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Mungu ana shoka lake na yuko tayari kukata na kuchoma mti wowote unaozaa matunda mabaya" au "Kama vile mtu atayarishavyo shoka kukata na kuchoma mti ambao huzaa matunda mabaya, Mungu yuko tayari kuwaadhibu ninyi kwa ajili ya dhambi zenu."

kwa ajili ya toba

"kuonesha kwmba umekwisha tubu"

Lakini ajaye nyuma yangu

Yesu ni mtu yule ambaye anakuja nyuma ya Yohana

ni mwenye uwezo kuliko mimi

'ni wa muhimu zaidi kuliko mimi"

Atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto

Sitiari hii hulinganisha ubatizo wa Yohana wa maji kwa ubatizo ujao wa moto. Hii humaanisha ubatizo wa Yohana kiishara huwatakasa watu dhambi zao. Ubatizo kwa Roho Mtakatifu na moto utatakasa dhambi za watu kwa kweli. Kama inawezekana, tumia neno "batiza" katika tafsiri yenu kutunza ulinganishaji wa ubatizo wa Yohana.

Pepeto lake li mkononi mwake kupepeta ngano

Sitiari hii hulinganisha namna Kristo atakavyo watenganisha watu wenye haki na watu wasio haki kwa namna mtu atenganishavyo nafaka ya ngano na makapi. "Kristo ni kama mtu ambaye pepeto lake liko mkononi mwake."

Pepeto lake li mkononi mwake

Hapa "mkononi mwake" humaanisha mtu yuko tayari kutenda. "Kristo ameshikilia pepeto kwa sababu yuko tayari."

pepeto

Hiki ni kifaa kwa ajili ya kurusha juu hewani kutenganisha nafaka za ngano na makapi. Nafaka zenye uzito hurudi na kuanguka chini na makapi yasiyotakiwa hupeperushwa na upepo. Kina fanana na umbo la uma ya nyasi lakini kina meno mapana kimetengenzwa kutokana na mbao.

sakafu yake ya kupuria

"kiwanja chake" au " kiwanja mahali ambapo hutenganisha nafaka na makapi"

kukusanya ngano yake katika ghala...kuchoma makapi kwa moto usioweza kuzimika

Hii ni sitiari inayoonesha jinsi Mungu atakavyowatenganisha watu wenye haki na watu waovu. Wenye haki wataenda mbinguni kama ngano katika ghala ya mkulima, na Mungu atawachoma watu ambao ni kama makapi kwa moto ambao hautazimika.

hautaweza kamwe kuzimika

Hii inweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kamwe hautazimika."