sw_tn/mat/02/01.md

1.5 KiB

Taarifa kwa ujumla:

Sehsmu mpya ya habari huanza hapa na kuendelea hadi mwisho wa sura. Mwandishi anasimulia kuhusu jaribio la Herode kumwua mfalme mpya wa Wayahudi.

Bthlehemu ya Yuda

"mji wa Bethlehemu katika jimbo la Uyahudi"

katika siku za mfalme Herode

"wakati Herode alipokuwa mfalme huko"

Herode

Hii humaanisha Herode Mkuu.

mamajusi

"watu wenye elimu ya nyota"

kutoka mashariki

"kutoka nchi ya mbali mashariki ya Uyahudi.

Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?

Watu wale walijua kutokana na elimu ya nyota kwamba yule ambaye atakuja kuwa mfalme alikuwa amekwisha zaliwa. Walikuwa wanajaribu kuchunguza mahali alipokuwa. Mtoto mdogo ambaye atakuja kuwa mfalme wa Wayahudi amezaliwa. Yuko wapi?"

nyota yake

Walikuwa hawasemi kwamba mtoto mdogo alikuwa mmiliki halali wa nyota. "nyota ambayo hutuambia kuhusu yeye" au "nyota ambayo imehusishwa na kuzaliwa kwake.'

mashariki

"ilikuja tokea mashariki" au wakati tulopkuwa katika nchi yetu"

abudu

uwezekano wa maana ni 1) walikusudia kumwabudu mtoto mdogo kama Mungu, au 2) walitka kumpa heshima kama mfalme wa kibinadamu. Kama lugha yako ina neno ambalo huhusisha maana zote mbili, unapaswa kuzingatia kulitumia hapa.

alifadhaika

"alitaabishwa." Herode alitaabishwa kwamba mtoto mdogo huyu atachukua nafasi yake kama mfalme.

Yerusalemu yote

Hapa "Yerusalemu" ina maanisha watu. Pia "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anaongeza chumvi kusisitiza watu wangapi walitaabishwa. "watu wengi wa Yerusalemu."