sw_tn/job/20/28.md

1.1 KiB

Habari za Jumla:

Sehemu hii ni hitimisho la hotuba ya Sofari kwa Ayubu.

toweka

"kutoonekana" au "enda mbali"

bidhaa zake zitamwagika mbali

Maneno "mwagika mbali" yanawakilisha kuondolewa mbali kutoka kwake."bidhaa zake zitachukuliwa mbali kutoka kwake, kama bidhaa zinazoelea katika mafuriko"

siku ya ghadhabu ya Mungu.

Neno "ghadhabu" linawakilisha kuadhibiwa. Kielezi cha jna "ghadhabu" chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "adhibu""siku ambayo Mungu huwadhibu watu"

Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu,

Maneno "sehemu kutoka kwa Mungu" yanawakilisha kile ambacho Mungu amekikusudia kitokee kwa mtu fulani. Kimezungumzwa kana kwamba kilikuwa kitu ambacho Mungu angempa yeye. "Hiki ndicho ambacho Mungu amekikusudia kitokee kwa mtu mwovu"

urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye."

Tungo hii inawakilisha kile ambacho ameamua kinapaswa kitokee kwa mtu fulani. Kimezungumzwa kana kwamba kilikuwa kitu ambacho Mungu angempa yeye hapo kabla kama urithi. "Kile ambacho Mungu amekipanga kumpa yeye" au "kile ambacho Mungu amekikusudia lazima kitokee kwake"