sw_tn/job/18/03.md

2.1 KiB

Habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama

Bildadi anatumia swali hili la kejeli kusisitiza kwa Ayubu kuwa hapaswi kufikiria kuwa ni mpumbavu. Yeye anazungumzia wao kufikiriwa kuwa ni wapumbavu kwa kuwaita "wanyama hatari wa porini." Swali hili laweza kuandikwa billa hali ya kuuliza ikasomeka hivi: Wewe hupaswi kufikiri kuwa sisi ni wanyama hatari wa porini." au "Wewe hupaswi kufikiri kuwa sisi ni wapumbavu kama wanyama"

Kwa nini sisi

Neno "sisi" huenda lina maanisha Bildadi na rafiki wengine wa Ayubu.

kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?

Bildadi anatumia swali hili la kejeli kwamba yeye hapaswi kuwafikiria wao kuwa ni wapumbavu."Sisi hatuko wapumbavu kama wewe unavyofikiri kuwa tuko hivyo"

machoni pako?

Katika sentensi hii neno uoni linawakilisha hukumu au tathimini. "katika hukumu yako"

Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako

hapa Bildadi anasema kwamba ni kwa sababu ya hasira ya Ayubu na kutokuwa mtiifu kwa hiyo amejeruhiwa, siyo kwa sababu ya hasira ya Mungu kama vile alivyodai hapo kabla. Neno "rarua" hapa linamaanisha "jeruhi" "Wewe umesababisha kujeruhiwa kwako kwa sababu ya hasira"

nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?

Swali hili la kizushi linasema kwamba kumwacha Ayubu ambaye wanamfikiria kuwa ni mtu mwenye hatia, aende kwa uhuru itakuwa kama kuubadilisha ulimwengu wote. Ayubu anatumia lugha ya kukuza sana jambo jinsi gani inavyoshangaza waanavyofikiri jinsi iliyo. Swali hili laweza kuandikwa billa hali ya kuuliza ikasomeka hivi: Kumwomba Mungu akuache wewe, mtu mwenye hatia, uende kwa uhuru ni kama upumbavu, kama kuiomba ardhi kusamehewa kwa faida yako au kwa ajili ya Mungu kuhamisha miamba kutoka mahali pake kukufurahisha wewe"

nchi inapaswa kusamehewa

"kila mmoja anapaswa kuiacha nchi"

miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?

Neno "mwamba" katika sentensi hii lina maanisha miamba mikubwa, kama vile milima. "Mungu anapaswa kuihamisha milima kutoka mahali pake " au"Mungu aihamishe milima inayozungunguka mahali pale"