sw_tn/job/17/13.md

1.9 KiB

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu;

"Kutazama" ina maanisha "kufikiri" kwa jinsi hiyo. Mimi ninafikiri juu ya kuzimu kama nyumbani kwangu" au "Mimi sasa nafikiri kuzimu ni nyumbani kwangu mimi"

Mimi nimetandaza kiti changu katika giza;

Sentensi hii ina maanisha Ayubu kuwa amejiandaaa kufa kama vile kuwa amekitandika kitanda chake yeye katika giza." "nimejiandaa mwenyewe kwenda na kulala miongoni mwa waliokufa"

nimetandaza kiti changu

"nimekitengeneza kitanda changu"

Mimi nimesema na shimo....na kwa funza,

Mistari hii miwili inatofautiana na imetumiwa kwa pamoja kusisitiza jinsi gani Ayubu alikuwa mkiwa"

shimo

"kaburi"

Wewe ni baba yangu

Ayubu anazungumzia ule ukaribu atakaokuwa nao hivi karibuni na kaburi lake akilinganisha na ukaribu wa mtu alio nao na familia yake"wewe uko karibu na mimi kama baba yangu" au"Wakati mimi nitakapozikwa, wewe utakuwa karibu na mimi kama baba"

funza

"wadudu wadogo." minyoo ambayo ni viumbe wadogo ambao hula miili iliyooza.

Wewe ni mama yangu au dada yangu;

Ayubu anazungumzia ule ukaribu atakaokuwa nao hivi karibuni na kaburi lake akilinganisha na ukaribu wa mtu alio nao na familia yake"wewe uko karibu na mimi kama mama yake na dada zake. "Wew uko karibu na mimi kama mama yangu na dada yangu" au"Wewe utakuwa karibu na mimi kama mama au dada"

liko wapi tena tumaini langu?

Jibu dhahiri ni "hakuna popote," kwa sababu hana tumaini. Swali hili la kejeli linaweza kuandikwa pasipo kutumia swali hivi: "Mimi sina tumaini"

Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?

Swali hili la kizushi limetumika kusisitiza kuwa hakuna mtu yeyote anayetarajia yeye kuwa na tumaini lolote. Swali hili la kejeli linaweza kuandikwa bila kutumia swali hivi: "hakuna awaye yote anayeweza kuona tumaini kwangu" au "Hakuna ategemeaye mimi kuwa na tumaini lolote"