sw_tn/job/11/07.md

1.2 KiB

Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?

Haya maswali mawili ya mfano yanauliza kitu kile kile. Mwandishi anatumia mfumo wa maswali kuongeza msisitizo."Wewe huwezi kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye, na wewe hautaweza kabisa kumfahamu aliye mkuu"

Upeo

Hii inamaanisha kumfahamu Mungu.

uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe ? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu;

Kutokuweza kumfahamu Mungu kumezungumzwa kuwa kama vile ilikuwa haiwezekani kwenda mbali mahali pa kuzimu. "haifikiwi kama mahali pa juu mbinguni ....haifikiwi zaidi kuliko mahali pa chini pa kuzimu"

unaweza kufanya nini wewe ?

Sofari anatumia swali hili kuonyesha kuwa mtu hawezi kufanya chochote kumfahamu Mungu kabisa."wewe huwezi kufanya chochote" au " wewe huwezi kumfahamu yeye kikamilifu"

waweza kufahamu nini wewe?

Sofari anatumia swali hili kuonyesha kwamba mtu hawezi kumfahamu Mungu kwa ukamilifu."Wewe huwezi kumfahamu Mungu kwa ukamilifu" au wewe huwezi kufahamu yale yote ya kufahamu"

Vipimo vyake

Ukuu wa Mungu, au ukuu wa hekima

ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.

Ukuu wa Mungu au hekima umezungumzwa kama unaweza kupimwa katika umbali.