sw_tn/job/10/04.md

1.1 KiB

Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?

Mswali haya mawili yanamaana zinazo karibiana. Maswali haya yatarajia jibu hasi kusisitiza kwamba Mungu haoni au kuelewa mambo kama vile mtu aelewavyo. Yanaweza kuelezewa kama habari. "Wewe huna macho ya mwili, na hautazami kama mtu atazamavyo."

Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu ... na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?

Swali hili linatarajia jibu hasi kusisitiza kwamba Mungu ni waa milele na siku za mtu ni ndogo. Linaweza elezewa kama habari. "Siku zako si kama siku za mwanadamu na miaka yako si kama miaka ya watu ... na hapana yeyote ambaye ataweza kuniokoa mkoni mwako."

siku zako ni kama siku za wanadamu ... miaka yako ni kama miaka ya watu

Vifungu hivi viwili vina maana zinazokaribiana.

siku zako

"hesabu ya siku zako"

miaka yako

"hesabu ya miaka yako"

ukauliza habari za uovu wangu ...kutafuta dhambi yangu

Vifungu hivi viwili vinamaana zinazo karibiana.

hata ukauliza

"tena ukatafuta"

kutoka mkoni mwako

Hapa "mkono wako" ni mfano nguvu za Mungu. "kutoka nguvuni mwako"