sw_tn/job/07/11.md

761 B

Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu

Ayubu anawasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kuelezea sababu za yeye kutokukaa kimya.

sitakizuia kinywa changu

"Mimi sitaacha kuongea"

maumivu makubwa ya roho yangu

"mateso ya moyo wangu" au "maumivu makali ya mateso yangu"

uchungu wa nafsi yangu

"uchungu wa moyo wangu"

Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?

Ayubu anatoa swali hili kuelezea hasira yake kwa Mungu. Kwa kujilinganisha yeye mwenyewe na bahari au kiumbe cha kutisha baharini, Ayubu anamaanisha kwamba Mungu anamchukulia yeye kama kiumbe cha kutisha. 'Mimi siyo bahari au kiumbe cha baharini ambacho huitaji mlinzi wa kukilinda."