sw_tn/job/06/21.md

1.2 KiB

Habari za Jumla:

Katika mistari hii, Ayubu anatoa maswali manne kuwakaripia rafiki zake na kusisitiza kwamba yeye hakuomba msaada kutoka kwa yeyote kati yao.

Kwa sasa

Ayubu anatumia kifungu hiki kuanza sehemu kuu ya kile anachosema.

ninyi rafiki si kitu kwangu

"hamtendi kama rafiki zangu"

nanyi mwaogopa

"na ninyi mnaogopa kwamba Mungu anaweza kuwafanyia mambo hayahaya." Hapa inaweka bayana zaidi habari ya kutisha kwamba rafiki zake wanaogopa kuadhibiwa na Mungu.

Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?'

"Sijamuomba yeyote kati yenu kitu chochote."

nitoleeni zawadi katika mali zenu?

"Mimi sijawaomba mnipe pesa." au "Mimi sijawaomba kutoa bibi harusi kwaajili yangu kutoka katika mali zenu."

Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?

"Mkono wa mtesi wangu" ni mfano ambao unasimama badala ya nguvu ya mtu fulani ambaye anashindana kwa nguvu sana na Ayubu. "Mimi sijawahi kumwomba mmoja kati yenu kuniokoa kutoka kwa adui zangu"

Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?

"Mkono wa mtesi wangu" ni mfano ambao unasimama badala ya nguvu za watu ambao wanamtendea Ayubu vibaya. 'Mimi sijawaomba kuniokoa kutoka kwa wale ambao wananitendea vibaya."

Niokoe

"nisaidie"