sw_tn/job/05/14.md

1.2 KiB

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mstari, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza namna Mungu anavyowashusha wale ambao ni werevu na kuwaokoa wale ambao ni masikini.

hupatwa na giza wakati wa mchana

Hapa mwerevu, watu waovu ambao Mungu amewachanganya wanazungumziwa kana kwamba bila matarajio wakawa gizani wakati wa adhuhuri, wakati jua likiwa sehemu ya katikati ya anga. Hawawezi kufanya chochote wanachotamani kufanya, kwasababu hawawezi kuona. "Wale ambao ni werevu wako gizani, hata wakati wa muda wa adhuhuri"

kupapasa

papasa kwa mikono pande zote kama mtu kipofu

wakati wa mchana

"saa sita mchana"

Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao

Hapa mambo ya matusi na vitisho ambayo watu husema yanazungumziwa kana kwamba ni upanga vinywani vyao. "Lakini humwokoa mtu masikini kutokana na vitisho vya mwenye uwezo" au "Lakini yeye humwokoa mtu masikini wakati mwenye uwezo anapowatisha au kuwatukana wao"

udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.

Watu ambao husema mambo yasiyo haki wanazungumziwa kana kwamba wao ni wadhalimu, ambao lazima waache kuongea. "Hata hivyo ni kama mdhalimu afunge mdomo wake."