sw_tn/job/01/09.md

1.9 KiB

Je Ayubu amcha Mungu bila sababu?

"Je Ayubu anamheshimu Mungu bila sababu?" Shetani akamjibu Mungu kwa kuwasilisha na kujibu maswali yake mwenyewe. Akasema kwamba Ayubu anamheshimu Mungu tu kwa sababu Mungu anambariki yeye. "Ayubu ana sababu ya kumtii Mungu."

Wewe hukumwekea kinga pande zote, kuzunguka nyumba yake, na kuzunguka vitu vyote alivyo navyo kutoka kila upande

Shetani anaeleza ukweli kuunga mkono hoja yake. "Wewe umemlinda yeye, familia yake na kila kitu anachomiliki."

kumwekea kinga pande zote, kuzunguka nyumba yake

kama kizuizi kama vile ukuta au uwa wa miti iliyooteshwa kuzunguka na kulinda ardhi ya mtu, Mungu amemzungushia Ayubu na ulinzi wake. "akamlinda yeye na nyumba yake"

kazi za mikono yake

"Kila kitu ambacho anafanya"

mifugo yake imeongezeka katika nchi

"ana mifugo zaidi na zaidi katika nchi"

Lakini sasa nyosha mkono wako na uguse yote hayo aliyonayo, na uone kama hatakufuru mbele ya uso wako.

Shetani anamaanisha kwamba kama Mungu atamshambulia Ayubu, ataona namna ambavyo Ayubu atajibu. "Lakini sasa, kama utanyosha mkono wako na uguse vyote alivyonavyo, utaona atakavyo kufuru mbele ya uso wako"

Lakini sasa nyosha mkono wako

Hapa "mkono" unahusiana na uwezo wa Mungu wa kutenda. "Lakini sasa zitumie nguvu zako"

uguse yote hayo aliyonayo

Hapa "gusa" linawakilisha tendo la kudhuru au kuangamiza. "shambulia vyote alivyonavyo" au "angamiza vyote alivyonavyo"

ya uso wako.

Hii inahusu muda ambao Mungu yuko makini. "katika uwezo wake wa kusikia"

Tazama

"Tazama" au "kuwa makini na yote ambayo na kwenda kukuambia"

hayo yote aliyonayo yamo mkononi mwako

Hapa "mkono" unawakilisha uwezo wa mtu kudhibiti kitu fulani. "una uwezo juu ya yote aliyonayo."

juu yake yeye mwenyewe

"dhidi ya mwili wake" "lakini usimdhuru kimwili" au "usiudhuru mwili wake"

akatoka mbele za BWANA.

"aliondoka kutoka kwa BWANA" au "Akamwacha BWANA"