sw_tn/job/01/04.md

1.2 KiB

Kwa siku yake kila mtoto wa kiume, hufanya

Neno "siku" labda linahusu siku ambayo walisherehekea kuzaliwa kwa mtoto wa kiume. Lakini angalau inahusu wazo la kila mtoto wa kiume kuchukua mwelekeo katika kufanya sherehe. "Katika sherehe ya siku ya kila mtoto wa kiume, mwana hutoa" au " Kila mtoto wa kiume kwa upande wake hutoa"

hufanya ... Wakatuma ... Ayubu hutuma ... kuwatakasa ... Aliamka asubuhi na mapema ... na kusema

"kwa desturi alitoa ... kwa desturi walituma ... Ayubu kwa desturi alituma ... kwa desturi aliwaweka wakfu ... Kwa desturi aliamka mapema ... kwa desturi alisema"

yeye huwatakasa

Hapa "weka wakfu" humaanisha kumsihi Mungu kuondoa ibada yoyote chafu ambayo watoto wa Ayubu huenda waliileta juu yao wenyewe wakati wakisherekea kwa furaha pamoja. Ayubu alifanya haya kwa kuwatolea sadaka kwa Mungu.

pamoja nao

Neno "wao" linahusu watoto saba wa kiume na mabinti watatu lakini halimjumuishi Ayubu.

Baada ya siku za karamu zilipokuwa zimetimia

"Wakati sherehe zilipomalizika" au "Baada ya sherehe"

Ayubu hutuma kwao

"Kwa desturi Ayubu alituma mtu kuwaita waje kwake mwenyewe"

kumkufuru Mungu mioyoni mwao

Mara nyingi mawazo hayo huja bila kukusudia, bila mtu kusubiri kuyafikiri. "kumkufuru Mungu mawazoni mwao"