sw_tn/jas/05/19.md

1.2 KiB

Ndugu zangu

"Waamini wenzangu"

kama yeyote miongoni mwenu anapotoka kutoka kwenye ukweli, lakini mtu mwingine akamrejesha

Mwamini ambaye anaacha kumwamini Mungu na kumtii yeye anafananishwa na kondoo aliyeondoka kwenye kundi. Mtu anayemrejesha ili amwamini Mungu tena anafananishwa na mchungaji anayetafuta kondoo aliyepotea. "Mtu yeyote akiacha kumtii Mungu na mwingine akamsaidia kuanza kumtii Mungu tena"

yeyote amwongozaye mwenye dhambi kuondoka katika njia yake ya ukosaji... atafunika wingi wa dhambi.

Yakobo anamaanisha kuwa Mungu atatumia matendo ya huyu mtu ya kumrejesha aliyekosa ili atubu na kuokolewa. Lakini Yakobo anaongea kama vile huyu mtu mwingine ndo ameokoa nafsi ya mwenye dhambi toka kwenye kifo.

ataponya nafsi yake kutoka katika mauti na atafunika wingi wa dhambi.

Hapa "kifo" inamaanisha kufa kiroho, kutengana na Mungu. "Atamuokoa na kifo cha kiroho na Mungu atamsamehe mkosaji dhambi zake zote"

atafunika wingi wa dhambi.

Yawza kumaanisha kuwa 1) Mtu atakayemrejesha ndugu aliyetenda uovu, dhambi zake zitasamehewa. au 2) Ndugu aliyetenda uovu akirudi kwa Bwana , dhambi zake zitasamehewa. Dhambi inazungumzwa kama jambo ambalo Mungu atawasamehe watu wake.