sw_tn/jas/05/01.md

1.7 KiB

Sentensi unganishi

Yakobo anawaonya matajiri juu ya starehe na utajiri.

enyi mlio matajiri

Yaweza kuwa na maana ya 1) Yakobo anawapa onyo kali wale wanaoamini kwenye utajiri au 2) Yakobo anazungumza kuhusu watu wasioamini ambao ni matajiri. "enyi mlio matajiri na mnaosema mnamcha Mungu"

kwa sababu ya taabu inayokuja juu yenu

Yakobo anaelezea kuwa watu hao watateseka sana baadae na taabu yao inakuja. "kwa kuwa mtateseka sana baadae"

Utajiri wenu umeharibiwa na mavazi yenu yametafunwa na wadudu waharibifu. Dhahabu zenu na fedha zenu zimekosa thamani

imetafunwa. Dhahabu zenu na fedha zimekosa thamani. Yakobo anazungumza juu ya matukio haya kama vile yameshatokea. Yakobo anazungumzia utajiri wa duniani haudumu na hauna uzima wa milele. "Utajiri wenu umeharibiwa, nguo zenu zimetafuwa na dhahabu zenu na fedha zimekosa thamani"

utajiri ... nguo ... dhahabu

Hivi vitu vimetajwa kama mifano ya vitu vya thamani kwa mwanadamu.

uharibifu wake utashuhudia dhidi yenu

"uharibifu" ni neno linaloelezea namna ambavyo chuma yaweza haribika. Yakobo anazungumzia kuhusu uharibifu kwa kuwa umesababishwa na watu waovu na matendo yao. "Na Mungu akiwahukumu kuharibiwa kwa mali zenu kutakuwa kama mtu anayewahukumu mahakamani"

Itaangamiza ... kama moto

Uharibifu unazungumzwa kama vile moto ambao utakuja kuwaangamiza watu.

Miili yenu

"mwili" inamaanisha mwili mzima.

Moto

Moto inatumika kuwakumbusha watu kwamba mara nyingi inamaanisha hukumu ya Mungu itakayokuja juu ya waovu.

Katika siku ya mwisho.

Hii inaelezea wakati muafaka wa Mungu kuja kuhukumu ulimwengu. Waovu wanadhani wanahifadhi utajiri kwa ajili ya baadae lakini wanachokifanya wanahifadhi hukumu. "wakati ambao Mungu anataka kuwahukumu"