1.1 KiB
Enyi wazinzi
Yakobo anazungumza na waamini akiwafananisha na mke aliyelala na mwanaume mwingine ambaye sio mume wake. "ninyi sio waaminifu kwa Mungu"
Hamjui kwamba ... Mungu?
Yakobo alitumia hili swali kuifundisha hadhira yake. "Mnajua ... Mungu"
urafiki na ulimwengu
Maneno haya yanaelezea uhusiano uliopo kwenye mifumo ya duniani na tabia zake.
urafiki na ulimwengu
Hapa mfumo wa ulimwenguni unaelezewa kama vile ni mtu ambaye watu wengine wanaweza kuwa na urafiki naye.
urafiki na ulimwengu ni uadui dhidi ya Mungu
Kuwa rafiki na ulimwengu inamaanisha kuwa adui wa Mungu. "urafiki na dunia" inamaanisha watu ambao ni marafiki wa dunia na "uadui dhidi ya Mungu" inamaanisha watu ambao wanampinga Mungu. "Marafiki wa ulimwengu ni maadui wa Mungu"
Au mnadhani maandiko hayana maana
Yakobo anatumia swali kueleza kuwa "Kuna maana katika maandiko"
Roho aliyoweka ndani yetu
Tafisi nyingine zinaelezea "roho" kama Roho Mtakatifu. Na tafsiri zingine zinamaanisha roho ya binadamu ambayo kila mtu ameumbwa nayo. Tunapendekeza kuwa utumie maana nyingine ambayo ipo katika tafsiri zinazotumika na wasomaji wako.