sw_tn/jas/02/18.md

1.2 KiB

Bado mtu fulani anaweza kusema

Yakobo alikuwa anasahihisha uelewa wa hadhira yake juu ya imani na matendo.

Una imani, na mimi ninayo matendo

"Inakubalika iwapo mtu mmoja ana imani na mwingine ana matendo." Yakobo anaelezea ni kwa namna gani watu wnaweza kulumbana dhidi ya mafundisho yake.

Una imani, na mimi ninayo matendo ... nionyeshe imani yako

Yakobo anazungumzia imani na matendo kama vitu ambavyo watu wanaweza kuwa navyo na kuwaonesha wengine.

nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu

Yakobo anazungumza kuwa imani inaweza kuonekana endapo mtu atafanya matendo mema. "Nitaionesha imani yangu kwa kufanya matendo mema"

mapepo nayo yanaamini hivyo na kutetemeka.

"mapepo nayo yanaamini, lakini yanaogopa kwa hofu. Yakobo anafananisha mapepo na watu wanaosema wana imani lakini hawafanyi matendo mema. Yakobo anasema pepo wana busara maana wanamuogopa Mungu wakati watu hawamuogopi.

Je, unataka kujua, ewe mtu mpumbavu, namna ambavyo imani hiyo pasipo matendo isivyofaa?

Yakobo alitumia swali kuwakemea watu ambao hawakumsikiliza. "Ewe mpumbavu, hautaki kunisikiliza thibitisha namna isivyofaa imani bila matendo.

Je, unataka kujua ... isivyofaa?

"Nitawaonyesha ni jinsi gani ... isivyofaa."