sw_tn/jas/01/01.md

1.6 KiB

Sentensi unganishi

Baada ya salam zake za ufunguzi, Yakobo anawaambia waamini kwamba kusudi la majaribu ni kupima imani.

Yakobo, mtumishi wa Mungu na Bwana Yesu Kristo.

Neno "Niko" linamaanisha " Mimi, Yakobo ni mtumishi wa Mungu na Bwna Yesu Kristo"

Yakobo

Yakobo alikuwa ndugu yake na Yesu.

Kwa kabila kumi na mbili waliotawanyika.

Hii inaelezea eidha wayahudi wote wa Kikiristo waishio nje ya Israeli au Wakristo wote waishio popote duniani.

Makabila kumi na mbili.

Neno "makabila "kumi na mbili" yanamaanisha watu wote wa Israeli kwa kuwa waligawanywa katika makabila "kumi na mbili". Kwenye mistari hii makabila kumi na mbili yanamaanisha Wayahudi wote wa Kikristo au Wakristo wote duniani. Hapa neno "kumi na mbili" hutumika kama jina na namba "kumi na mbili" inapaswa kuandikwa kama neno sio kama namba.

Kutawanyika

Neno "kutawanyika" kunamaanisha Wayahudi wote waliotawanyika kwenye nchi nyingine mbali na nyumbani kwao Israeli. Kenye mistari hii "kutawanyika" linamaanisha Wakristo wa kiyahudi waishio nje ya Israeli au Wakristo wote waliopo popote duniani.

Salam

Salam ya kawaida kama "habari" au "siku njema".

Furahini ndugu zangu, mpatapo matatizo.

"Waamini wenzangu, yaone matatizo yote uliyonayo kama mambo ya kukufanya ushangilie"

Jaribu la imani yenu inatengeneza uvumilivu.

Maneno "jaribu", "imani yenu", na "kuvumilia" ni maneno yanayosimama kuonyesha matendo. Mungu hutujaribu ili kujua ni kwa namna gani tunamwamini yeye na kumtii. Waamini ("ninyi") mwamini yeye na mvumilie mateso. "Mnapokutana na magumu Mungu anagundua ni kwa kiasi gani unamwamini. Na matokeo yake unakuwa na uwezo wa kushinda majaribu magumu zaidi.