sw_tn/isa/62/03.md

706 B

Pia utakuwa taji la uzuri mikononi mwa Yahwe, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako

Hizi zina maana moja na zinaunganishwa kwa ajili ya msisitizo. Zinasema ya kwamba Yerusalemu utakuwa mji wa kifalme chini ya nguvu na mamlaka ("mkono") ya Mungu.

haitakuwa kwako tena ... kusemwa, "Ukiwa"

Hizi zina maana moja na zinaunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

haitasemwa kwako tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu hawatasema tena juu yako"

wala nchi yako haitasemwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wala watu hawatasema tena juu ya nchi yako"

na nchi yako itaolewa

Hii ina maana Yahwe atawapenda watu wa Israeli na atakuwa nao daima kama alivyo mume.