sw_tn/isa/57/14.md

701 B

Jenga, jenga! Safisha njia! Ondoa vitu vyote vya kujikwaa kutoka katika nja ya watu wangu

Yahwe ana nguvu na haraka ya kwamba njia ya wazi na tambarare iweze kuwepo kwa watu kurudi kwake na kufungulia vikwazo kwa kumuabudu Yahwe. Hii inaitikia 40:3.

Kwa maana hiki ndicho Yule aliye juu na kuinuliwa asemavyo

Maneno "juu" na "kuinuliwa" kimsingi ina maana moja hapa na inasisitiza Yahwe kuinuliwa.

kufufua roho ya wanyenyekevu, na kufufua moyo ya wenye majuto makali

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe atawatia nguvu na kutia moyo wale ambao wanajishusha mbele yake.

roho ... moyo

Hapa hizi zina maana ya mawazo ya mtu na hisia, sio roho na moyo kihalisia.